Mkuu
wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga SC, Jerry Muro ametoa
taarifa ya viingilio kwa mchezo wa keshokutwa dhidi ya FC PLATNUM ambapo
katika jukwaa la viti vya Rangi Chungwa itakuwa Sh, 7,000, VIP C Sh.
15,000, VIP B Sh. 20,000, na VIP A Sh 30,000.
Muro
amesema tiketi zitaanza kuuzwa Jumamosi Saa 2:00 asubuhi katika vituo
vya Karume (Ofisi za TFF), Mgahawa wa Steers (Posta Mpya), Oilcom
(Buguruni), BigBon (Kariakoo), Olicom (Ubungo), Dar Live (Mbagala),
Uwanja wa Uhuru, Kivukoni (Ferry) na Makumbusho (kituo cha
mabasi).Aidha, amesema magari yenye vibali maalum ndiyo yatakayoruhusiwa
kuingia ndani ya Uwanja siku ya Jumapili.
No comments:
Post a Comment